KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Monday 5 September 2011

Mjue Dr. Dalaly Peter Kafumu, Mgombea Ubunge Jimbo La Igunga Kwa Tiketi Ya CCM

JINA :Dk. Dalaly Peter Kafumu
 
KUZALIWA-Agosti 4, 1957        
 
MAHALI      
Kijiji cha Itumba, Tarafa ya Igunga Wilaya ya Igunga mkoani Tabora.
 
NDOA
              Nina mke  na watoto watano ambao kati yao watatu ni Madaktari wa binadamu, wengine wawili bado wanasomea Udaktari wa Binadamu na mmoja anasoma  Stashahada ya Ufamasia.
 
ELIMU
 *Shahada ya kwanza ya Madini- BSc (Geology)-1983
*Stashahada ya Elimu-PGD (Education)-1987
*Shahada ya Uzamili ya Madini-BSc (Geology)-1995
*Stashahada ya Utafutaji Madini-PGD (Mineral Exploration)-1991
* Sahahada ya Uzamivu ya Madini-Ph.D (Geology)-2000


UZOEFU CCM*
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa TANU (TYL) tawi la Itumba (1971-1972)
*Mjumbe wa Kamati ya Siasa na Halmashauri Kuu ya Tawi la CCM, Madini (1983-1992).
*Mjumbe wa Mkutno Mkuu wa Wilaya na mkoa wa Dodoma (1983-1992).
*Katibu wa Tawi la CCM, Madini Dodoma (1988-2011).
*Kada wa CCM (1988-2011).


UTUMISHI WA UMMA
*Kamishna wa Madini Tanzania (2006-2011)
*Mkuu wa Mawasiliano Wizara ya Nishati na Mdini (2004-2006)
*Mkuu wa Kitengo cha Uhamasishaji na Takwimu Wizara ya Nishati na Madini (2002-2004).
*Mtaalam Mwandamizi wa Madini (1993-2002)
*Mhadhiri Chuo cha Mdini Dodoma (1978-1992)
*Mtaalam wa Madini Wizara ya Nishati na Madini (1983-1987).


 TAALUMA
*Mtaalam Bingwa wa Madini Nchini.
*Mwanachama wa Chama Cha Wataalam wa Madini Tanzania na Afrika.
*Mjumbe wa (II)) Bodi  za Usajili wa Makandarasi (II) Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na Chuo Kikuu    cha Dodoma (UDOM). 
 
  MCHANGO KWA TAIFA
*Mtaalam wa Madini (1983-1987)
Nilishiriki kwenye utafutaji wa madini na kugundua machimbo mengi ambayo sasa yanachimbwa na kuleta mapato, ajira na kukuza uchumi wa taifa.
 
*Mhadhiri wa Chuo cha Madini (1987-1992)
Nilifundisha mafundi sanifu katika fani ya madini, zaidi ya wahitimu 1,000 wanalitumikia taifa katika nafasi nyingi serikalini na kwenye sekta ya madini nchini.
 
*Mhadhiri wa Nje wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (2004-2006)
Nilifundisha masuala ya Jiolojia ya Mazingira na kuhitimisha wanafunzi zaidi ya 500 ambao sasa wanalitumikia taifa na katika sekta mbalimbali nchini.
 
*Kamishna wa Madini (2006-2011)
Nimesimamia marekebisho ya sheria ya Madini ya mwaka 1998 ili kupata sheria ya mwaka 2010. Sheria mpya inahakikisha kwamba:-
(i) Serikali na Wananchi wanashiriki zaidi katika uwekezaji madini kwa kupata hisa kwenye migodi.
(ii) Wananchi wanaoishi kwenye maeneo ya migodi wanafidiwa vizuri, kujengewa makazi mazuri na kushiriki kwenye mradi husika.
 
(iii) Kampuni kulipa kodi na mrahaba kwa viwango vya juu zaidi.
 
(iv) Wachimbaji wadogo wanatengewa maeneo yao, kupewa leseni zenye muda mrefu ili waweze kupata mitaji kutoka kwenye taasisi za fedha;na
(v) Viwanda vya uongezaji thamani ya madini vinajengwa hapa nchini ili kuongeza ajira na kukuza uchuni; na
(vi)Madini ya vito (Almasi, Tanzanite, Ruby na mengineyo) yanachimbwa na Watanzania tu.


MCHANGO KWA IGUNGA
*Kamishna wa Madini (2006-2011)
(i) Nilisaidia wachimbaji wadogo nchi nzima kupata maeneo na viwanja kwa ajili ya uchimbaji madini.
 
Kwenye Wilaya ya Igunga nimewasaidia wachimbaji wadogo wa madini kuwapa leseni maeneo ya Bulangamilwa na Nanga.
(ii) Kuwapatia soko la dhahabu mjini Nzega na Dar es Salaam wachimbaji wadogo wa dhahabu wa wilaya ya Igunga.
 
(iii) Kuwashauri wachimbaji wadogo nchini na Igunga kuhusu umuhimu wa kufuata sheria na kanuni za madini ili wasidanganywe na watu wanaotumia sekta ya madini kutapeli na kuwaibia.
(v)Ofisi yangu kama Kamishna wa Madini ilikuwa wazi kwa wana Igunga wote kufika na kuopata ushauri, maelekezo na msaada waliohitaji.


HUDUMA KWA JAMII (2005-2011)
(i) kujenga Misikiti miwili katika Kata ya Itumba, kutoa vitabu vya rejea na kiada kwa shule kumi za sekondari wilaya ya Igunga:- Itimba, Igunga, Mwamashimba, Mwisi,Mwanzugi, Igurubi, Manshiku, Simbo na  Nanga.
 
(ii) Kufadhili vikundi vya kina mama, Kata ya Itumba, Kwaya za Madhehebu ya Kikristo Igunga mjini na Mwanzugi.
 
(iii) Nikiwa  mwanachama wa Igunga SACCOS nimekisaidia chama changu kwa ushauri wa kitaalam na kutoa ada na hisa na michango yangu kwa wakati.
(v) Nikiwa mlezi wa Vijana Kata za Mwamashimba na Itumba nilifadhili vifaa vya michezo (mipira, jezi na kombe) na kuendesha ligi ya mpira wa miguu katika kata hizo mwaka 2009-2010.
(vi) Nilitoa mchango wa sh. 800,000 kuchangia ujenzi wa visima virefu viwili Kata ya Itumbi.


HUDUMA KWA UMMA WA TANZANIA
*NikiwaMjumbe wa Bodi ya Makandarasi (2006-2011) nimesimamia kuandikisha makandarasi nchini wanaotoa huduma za ujenzi kwenye sekta ya barabara na majengo na nikiwa mjumbe wa Bodi ya Chuo Kikuu cha Dodoma (2009-2011) nilishiriki katika usimamizi wa chuo hicho ili kutoa viajana wasomi bora wa kulitumikia Taifa la Tanzania.

No comments:

Post a Comment