KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Tuesday 13 September 2011

Kampeni Za CCM Zinaendelea igunga

Dokii, akiwajibika jukwaani.
Katibu wa Uchumi na Fedha waCCM Taifa, Mwigulu Nchemba, akipokelewa na wanachama wa CCM,alipowasili kijijini Nkinga leo mchana kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mdogo wa chama hicho.
Katibu wa Uchumi na Fedha waCCM Taifa, Mwigulu Nchemba, akihutubia wananchi wa kijiji cha Nkinga leo mchana katika mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga. Akihutubia wananchi wa Nkinga, Nchemba aliwataka wakazi hao kumchagua mgombea wa CCM, Dr Dalali Kafumu, kuwa mbunge wao chama atokacho CCM, ndio chama pekee chenye sera  zinazotekelezeka. Aliwaasa wananchi wa Nkinga na Igunga kwa ujumla kutochagua wagombea wa vyama vya upinzania kwani vyama hivyo vipo kwa maslahi ya viongozi wake na sio kwa maslahi ya wananchi. "Ndugu zangu wana Nkinga, msithubutu kuchagua vyama vya upinzani, chagueni CCM kwa ajili ya mendeleo yenu. Chama cha CCM, ndicho chama pekee chenye sera zinazotekelezeka. Hawa wenzetu wapinzani hawa, hawana lolote. Vyama vyao ni porojo tupu. Vipo kwa maslahi ya viongozi tu na sio kwa maslahi ya wananchi wa Tanzania."
Katibu wa Uchumi na Fedha waCCM Taifa, Mwigulu Nchemba akimvisha bendera mwanachama mpya wa CCM, aliyejiunga kutoka chama cha CUF leo mchana katika mkutano wa kampeni wa kijijini Nkinga.
Hafsa Kazinja alikuwepo kutoa burudani kwa wanachama, wapenzi na mashabiki wa chama cha CCM.
Shabiki wa Chama Cha Mapinduzi akiwa kwenye Kampeni igunga.Picha Zote na Mdau Victor Makinda-igunga

No comments:

Post a Comment