KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Tuesday 6 September 2011

Rais Jakay Kikwete Aizawadia NSSF Kwa Mchango Wake Katika Sekta Ya Ujenzi Nchini

 Rais Jakaya Kikwete akihutubia katika ufunguzi wa mkutano wa siku tatu unaojumuisha wahandisi, Wabunifu majengo, Wakadiriaji na Makandarasi uliofanyika Mlimai City Jijini Dar es salaam jana
Rais Jakaya Kikwete leo amemkabidhi Cheti Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dr. Ramadhani Dau kwa kutambua mchango mkubwa wa Mfuko huo katika sekta ya ujenzi hapa nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dr. Ramadhani Dau akiwa mwenye furaha mara baada ya kukabidhiwa cheti na Rais Jakaya Kikwete kwa kutambua mchango mkubwa wa Mfuko huo katika sekta ya ujenzi nchini
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dr. Ramadhani Dau(Wa Pili Kushoto) akiwa wkenye mkutano huo jana jijini Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika Picha ya pamoja Mara baada ya kufungua Mkutano wa wahandisi, Wabunifu majengo, Wakadiriaji na Makandarasi uliofanyika Mlimai City Jijini Dar es salaam jana
 
Na Alfred Ngotezi
 
Rais Jakaya Kikwete leo amemkabidhi Cheti Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Dr. Ramadhani Dau kwa kutambua mchango mkubwa wa Mfuko huo katika sekta ya ujenzi hapa nchini.
 
Rais Kikwete ambaye alikuwa mgeni kwenye ufunguzi wa Mkutano wa siku tatu uliojumlisha wahandisi, Wabunifu majengo, Wakadiriaji na Makondrasi alitoa zawadi hiyo kwa niaba ya Bodi ya Wakondrasi.
 
Mkutano huo uliohudhuriwa na maelfu ya watu, kutoka nje na ndani, ulianza tarehe 5 na utakwisha tarehe 7 Septemba mwaka huu. Baadhi ya wajumbe walitoka Afrika Kusini, Zambia, Kenya na Malawi.
 
Akiongea kwenye hafla hiyo fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City mjini Dar es Salaam, Rais aliwapongeza Wahandisi, Wabunifu Majengo, Wakadiriaji na Makondrasi walioandaa mkutano huo na kuwataka wajiunge pamoja ili waweze kupata uwezo mkubwa wa kufanya kazi.
 
Katika siku za karibuni NSSF imekuwa na miradi mikubwa ya ujenzi. Baadhi ya miradi hiyo ni ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma, nyumba za Polisi Dar es Salaam na Zanzibar na nyumba za Jeshi huko Monduli Arusha. Hivi karibuni NSSF itaanza kujenga Daraja la Kigamboni.

No comments:

Post a Comment