KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Monday 5 September 2011

VODACOM MISS TANZANIA KUONDOKA NA GARI AINA YA JEEP MPYA YENYE THAMANI YA SHILINGI M.72


Meneja Masoko wa CFAO Motors Alfred Minja kulia na Mkuu wa Udhamini na Masoko Vodacoma Tanzania George Rwehumbiza wakifunua gari aina ya JEEP ambalo limetolewa kama zawadi ya Vodacom Miss Tanzania 2011 lenye thamani ya shilingi milioni 72 za kitanzania gari hilo limetengenezwa nchini Marekani. Hafla ya kuonyesha gari hilo la zawadi imefanyika asubuhi hii katika duka la kampuni ya CFAO Motors lililopo Barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam, kulia anayeshuhudia tukio hilo ni mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga.
Meneja Masoko wa CFAO Motors Alfred Minja katikati na Mkuu wa Udhamini na Masoko Vodacoma Tanzania George Rwehumbiza wakikabidhi funguo za gari lililotolewa na kampuni hiyo kama zawadi ya Vodacom Miss Tanzania kwa Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga
Warembo watakaoshindania taji la Vodacom Miss Tanzania wakiwa wamelizunguka gari ambalo lilmetolewa kama zwadi ya mshindi atakayeibuka siku hiyo.
Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wakifurahia zawadi yao gari aina ya Jeep iliyotolewa na wadhamini wa shindano hilo CFAO Motors na Vodacom Tanzania.

No comments:

Post a Comment