KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Wednesday 14 September 2011

Viongozi na Wananchi Watembelea Makaburi Ya Wahanga Wa Meli Zanzibar

MAKABURI  ya Wahanga wa ajali meli katika Kijiji cha Kama nje kidogo ya mjini wa Zanzibar Wilaya ya Magharibi. ambayo yamezikwa jumla ya miili ya watu 46 wakiwemo Watoto 23 na watu wazima 23.  
SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Pandu Ameir Kificho akiongoza na Ujumbe kutoka Arusha wa timu ya Wazee Sport Club ukiongozwa na Mwenyekiti wa timu hiyo Aatsa Atogho(kushoto), wakisoma dua katika makaburi ya wahanga wa ajali ya meli yaliyoko Kama Mkoa wa Mjini Magharibi.
MKUU wa wilaya ya Magharibi Unguja, Hassan Mussa Takrima, akitowa maelezo kwa Ujumbe wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa na Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mkama, walipotembelea eneo lilozikwa maiti wa ajali ya meli ya MV.Spice Kama wilaya ya Magharibi jana.
SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Pandu Ameir Kificho  akiuongoza Ujumbe kutoka Arusha wa Timu ya Wazee Sport Club ukiwa na Mwenyekiti wa timu hiyo Aatsa Atogho, mwenye suti nyeusi wakizuru makaburi ya Wahanga wa ajali ya meli Kama.Picha Zote na Othman Mapara-Zanzibar

No comments:

Post a Comment