KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Tuesday 23 August 2011

Rais Jakaya Kikwete Akutana Mchezaji maarufu wa Mpira wa Kikapu Nchini Marekani Dwight Howard Wa Orlando Magic

Mchezaji maarufu wa mpira wa Kikapu duniani Dwight Howard akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete zawadi ya jezi wakati nyota huyo alipomtembelea Rais ikulu jijini Dar es Salaam jana.Dwight Howard ni mchezaji nyota wa timu ya kikapu ya Orlando Magic ya nchini Marekani.
Nyota mchezo wa kikapu nchini Marekani Dwight Howard akimwangalia Simba aliyekaushwa kitaalamu na kupamba lango la Ikulu jijini Dar es Salaam huku akifurahia jambo na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati nyota huyo alipokwenda Ikulu kumsalimia Rais na kutoa ahadi ya kutoa msaada ili kukuza vipaji vya mchezo huo nchini.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete(kulia),Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na nyota wa mchezo wa kikapu nchini Marekani Dwight Howard(Katikati)wakati nyota huyo alipomtembelea Rais Ikulu jijini Dar es Salaam jana.Nyota huyo anachezea klabu ya Orlando Magic.Picha na Freddy Maro-IKULU

No comments:

Post a Comment