KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Sunday 21 August 2011

MAKAMU WA RAIS DK GHARIB BILAL MGENI RASMI FAINALI ZA MASHINDANO YA KUHIFADHI QUR-AN AFRIKA MASHARIKI NA KATI

Mshiriki wa mashindano ya kuhifadhi Qur-an, ambaye alishika nafasi ya pili katika mashindano hayo, Kombo Bahi Makame kutoka Unguja-Tanzania, akishiriki mashindano hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo Agosti 21, ambapo mgeni rasmi katika fainali hiyo  iliyowashirikisha washiriki 14 kutoka nchi za Afrika Mashariki na kati, alikuwa ni  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Mshiriki kutoka Tanzania, Ibrahim Ramadhan, akishiriki fainali za mashindano hayo katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam leo.
Mshiriki wa mashindano ya kuhifadhi Qur-an, ambaye alishika nafasi ya kwanza  katika mashindano hayo,  Jahuddin Adam,  kutoka Sudan  akishiriki mashindano hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo Agosti 21, ambapo mgeni rasmi wa fainali hiyo iliyowashirikisha washiriki 14 kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati, alikuwa ni  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Mshiriki wa mashindano ya kuhifadhi Qur-an, ambaye alishika nafasi ya tatu  katika mashindano hayo,  Mohammad Sad Tawfiq,  kutoka Egypt  akishiriki mashindano hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo Agosti 21, ambapo mgeni rasmi wa fainali hiyo iliyowashirikisha washiriki 14 kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati, alikuwa ni  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma Hotuba yake  wakati wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, leo Agosti 21, na kushirikisha jumla ya wshiriki 14 kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi , Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, wakati wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, zilizofanyika leo Agosti 21 kwenye ukumbi wa Diamondi Jubilee jijini Dar es Salaam, na kuwashirikisha washiriki 14, kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, wakati wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, zilizofanyika leo Agosti 21 kwenye ukumbi wa Diamondi Jubilee jijini Dar es Salaam, na kuwashirikisha washiriki 14, kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi, mshindi wa kwanza wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, Jahuddi n Adam, kutoka Sudan, baada ya kutangazwa mshindi wa fainali hizo, zilizofanyika leo Agosti 21 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, wakati alipowasili kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo Agosti, 21, kuhudhulia Fainali ya mashindano ya kuhifadhi  Qur-an tukufu iliyofanyika kwenye ukumbi huo na kuwashirikisha washiriki kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, wakiwa katika ukumbi wa Diamondi Jubilee jijini Dar es Salaam, leo Agosti 21 wakifuatilia kwa makini fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi na baadhi ya Viongozi wa dini ya Kiislamu, wakiwa katika picha ya pamoja na washindi wa kwanza hadi wa tatu wa fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, baada ya kutangazwa washindi hao katika ukumbi wa Diamond Jubilee leo Agosti 21.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi na baadhi ya Viongozi wa dini ya Kiislamu, wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa  fainali za mashindano ya kuhifadhi Qur-an, baada ya kumalizika kwa mashindano hayo  katika ukumbi wa Diamond Jubilee leo Agosti 21. Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi Ya Makamu Wa Rais

No comments:

Post a Comment