Kilimanjaro stars jana ilingaraa baada ya kuwalaza 2-0 timu ya Sudan iliyotoka kwenye mashindano ya Afcon hivi karibuni yalofanyika Gabon na Equatorial Guinea.
Magoli yote mawili yalitiwa kimyani na John Rafael Bokho huku pasi zote zilizaa zaa magoli zikitoka kwa Mrisho Ngasa.
Mpaka Kilimanjaro stars inaanza mashindano jana wachezaji Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatha wote wakichezea TP Mazembe ya Congo walikuwa bado hawajawasili.
Kocha wa Kili Star Kim Poulsen amesema “hilo nimewaachia TFF wafatilie na tunatarajia watakuja, ila kwasasa hatuwezi kulalamikia kutokuwepo kwao sababu tunao wachezaji wengine katika timu”