KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Tuesday 6 November 2012


Dkt.Bilal Afungua Mkutano Wa Bima

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia ngoma ya asili wakati akiwasili kwenye Ukumbi wa Blue Peal, jijini Dar es Salaam, leo kwa ajili ya kufungua mkutano wa 8 wa Kimataifa wa Bima, ulioanza leo Novemba 6, 2012 ukitarajia kumalizika Novemba 8, mwaka huu.
 Baadhi ya washiriki wa Mkutano huo wa Kimataiafa wa Bima, kutoka mataifa mbalimbali wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akihutubia, katika ukumbi wa Blue Peal, leo Novemba 6, 2012
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua mkutano wa 8 wa Kimataifa wa Bima, ulioanza leo Novemba 6, 2012 katika ukumbi wa Blue Peal, jijini Dar es Salaam. Mkutano huo unatarajia kumalizika Novemba 8 mwaka huu. Picha na OMR 

No comments:

Post a Comment