Kichwa cha treni pamoja na mabehewa sita ya awamu ya kwanza, yakisubiri kufanyiwa majaribio kwa Safari zitazoanzia Station Dar es Salaam mpaka Ubungo mnamo mwezi wa kumi, majaribia hayo yameongozwa asubuhi ya leo na Naibu Waziri wa Uchukuzi,Mhe. Dk Charles Tizeba (Mb) ambaye alipanda treni hiyo kuanzia Station Dar es Salaam Mpaka Ubungo.Serikali imetumia kiasi cha Sh. Bil 4.75 kwa ajili ya ukarabati wa njia, injini na mabehewa. (picha: Raha za Pwani Blog)
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Charles Tizeba (Mb) dirisha la pili kutoka kulia, akiangalia nje wakati wa majaribio ya mabehewa sita kati ya kumi na mbili yatakayofanya safari zake kutoka Station mpaka Ubungo kuanzia mwezi wa Kumi mwaka huu,Treni hizo zitasaidia wananchi katika usafiri jijini Dar es Salaam. (picha: Raha za Pwani Blog)
No comments:
Post a Comment