UZINDUZI WA TIGO MAMA AFRIKA SARAKASI WAFANA JIJINI DAR
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Leonard Thadeo kutoka Wizara ya Habari, vijana , utamaduni na michezo akizungumza machache katika ufunguzi wa maonyesho ya Tigo Mama AfriKa sarakasi yanayoendelea katika ukumbi wa ukumbi wa Mancom Centre ndani ya New World Cinema Mwenge. Maonyesho hayo yataendelea mpaka Oktoba 4, 2012.
Mkurugenzi wa Mancom Centre, Constantine Magavilla akiwakaribisha na kuwashukuru wageni waliokuwa wamefika katika uzinduzi wa Tigo Mama Afrika Sarakari.
Moja ya michezo iliyovutia katika Tigo Mama Africa Circus inayoendelea katika ukumbi wa Mancom ndani ya Centre New World Cinema Mwenge.
Michezo ya kamba nayo ilikuwa ya kuvutia.
Mchezo mwingine ulikuwa kurushiana vikapu kwa kutumia miguu.
Vijana wakionyesha uhodari wao wa kupaa juu.
Vijana wakiaga mara baada ya onyesho kumalizika.
Wanamuziki wa Bendi ya Inafrika nao wakiaga, kazi yao kubwa ilikuwa ni kusherehesha wakati vijana wakiendelea na onyesho.
Umati mkubwa wa watu uliojitokeza katika maonyesho hayo.
watu walipata fursa ya kubadilisha mawili matatu. Picha zote na Cathbert Angelo Kajuna wa www.kajunason.blogspot.com
No comments:
Post a Comment