KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Monday 30 July 2012

Mke Wa Waziri Mkuu.Mama Tunu Pinda Azindua Mradi Wa Maji Hospital Ya Mawenzi
Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda akifunua pazia pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya bia ya Serengeti SBL anayemaliza muda wake Bw. Richard Wells kama ishara ya uzinduzi rasmi wa mradi wa maji katika hospitali ya mkoa wa Kilimanjaro Mawenzi mjini Moshi, mradi huo ambao umefadhiliwa na kampuni ya bia ya Serengeti SBL umegharimu zaidi ya milioni 55 za kitanzania ulilenga kutoa suluhisho la muda mrefu katika matatizo sugu yayoikumba jamii hususani tatizo la uhaba wa maji safi kwa maendeleo ya maisha ya mtanzania, Kushoto katika picha ni Mkuu wa Wialaya ya Moshi Dk Msengi na yana uwezo wa kuhifadhi lita elfu 40.000 kwa wakati mmoja
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti B. Teddy Mapunda akitoa maelezo ya mradi huo kwa mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Bw. Richard. Wells anayemaliza muda wake.
Mkurugenzi mpya wa kampuni ya Bia ya Serengeti SBL Bw. Steve Gannon akifungua bomba la maji mara baada ya mama Tunu Pinda anayeshuhudia tukio hilo kuzindua mradi huo kwenye hospitali ya Mkoa ya Mawenzi mjini Moshi leo, wapili kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Moshi Dk Msengi na kushoto ni Mkurugenzi wa Serengeti SBL anayemaliza muda wake Bw. Richard Wells.
Mke wa Waziri Mkuu mama Tunu Pinda akizungumza katika uzinduzi huo huku wakuu wa kampuni ya bia ya Serengeti wakimsikiliza kutoka kushoto ni Teddy Mapunda Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko, Mkurugenzi Mtendaji mpya wa SBL Bw. Steve Gannon na Mkurugenzi Mtendaji anayemaliza muda wake Richard Wells.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Leonidas Gama akitoa hotuba yake katika uzinduzi huo huku mgeni rasmiMama Tunu Pinda akifuatilia kwa makini.
Kutoka kulia ni Nandi Mwiyombela Meneja Miradi Endelevu na uwajibikaji Bw. Malisa, Imani Lwinga Meneja Mawasiliano na Mtaalamu Masuala ya Fedha SBL Bw. John Collins.
Haya ndiyo Matenki ya maji katika mradi huo yataweza kuhifadhi lita elfu 40.000 za maji.
Mmama Tunu Pinda akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye hospitali ya Mawenzi kwa ajili ya kuzindua mradi wa maji kutoka kulia ni Mkurugenzi mpya wa SBL Bw. Steve Gannon, Mkurugenzi wa SBL anayemaliza muda wake B. Richard Wells na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Leonidas Gama.
Mama Tunu Pinda akisalimiana na Mkurugenzi wa SBL anayemaliza muda wake Bw. Richard Wells mara baada ya kuwasili kwenye Hospitali ya Mawenzi kwa ajili ya uzinduzi wa mradi wa maji, kulia ni Teddy Mapunda Mkurugenzi wa Mawasiliano SBL na Mkurugenzi mpya wa kampuni hiyo Bw. Steve Gannon.
Kutoka kulia ni Mganga mkuu wa Mkoa wa Kiliamjaro Dk Mtumwa Mwako Steve Gannon, Richard Wells na Teddy Mapuinda wakimsubiri mgeni rasmi.

Mgeni rasmi mama Tunu Pinda akiwasili katika eneo la Tukio.
Mama Tunu Pinda akisalimiana na Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti SBL Bw. Ephraim Mafuru.
Baadhi ya wauguzi na wageni mbalimbali waliohudhuria kwenye uzinduzi huo.
Teddy Mapunda akizungumza katika uzinduzi huo.
Bw. Richard Wells naye akatoa neno.
Wakuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti mstari wa mbele ni kutoka kulia ni Mkurugenzi mpya wa Kampuni ya Serengeti SBL Bw. Steve Gannon na Teddy Mapunda mstari wa nyuma kutoka kulia John Collins Mtaalam wa Fedha, Nandi Mwiyombela Meneja Miradi Endelevu na Uwajibikaji na Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko.
Mama Tunu Pinda akimsikiliza Bw. Richard WellsMkurugenzi wa SBL wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji katika hospitali ya Mawenzi leo.
Mkurugenzi wa Masoko SBL Bw. Ephraim Mafuru akizungumza katika mkutano huo.
Mama Tunu Pinda akipanda mti katika hospitali ya Mawenzi mara baada ya kuzindua mradi wa maji hospitalini hapo.
(picha zote kwa hisani ya Fullshangwe )

No comments:

Post a Comment