KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Thursday 19 July 2012


Baadhi ya miili ya maiti ya waliookolewa kutoka katika MV Skagit iliyozama hapo jana, wakitambuliwa na ndugu zao katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar, na kuruhusiwa kuichukuwa kwa ajili ya taratibu za mazishi.
Balozi wa Marekani Nchini Tanzania, Lenhardt Alfonso wakatikati akionekana na huzuni Baada ya kuziona Maiti zilizookolewa katika Meli iliozama hapo jana katika Bahari ya Chumbe Zanzibar.Balozi alifika katika Viwanja vya Maisara ili kuona namna shughuli za kushughulikia maiti zinavyoendelea.
Mama alietambulika kwa Jina la Bitatu Uyelo ambae amenusurika na kupoteza mtoto wake wa miezi tisa katika ajali ya MV Skagit.
Waziri wa Mambo ya ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emanuel Nchimbi alifika katika eneo lililohifadhiwa Maiti wa ajali ya MV Skagit ili kutambuliwa na ndugu zao na kupata maelezo kwa Daktari Kiongozi (hayupo pichani) katika Viwanja Vya Maisara Zanzibar.
Baadhi ya Maiti waliookolewa kutoka katika MV Skagit na kukosa watu wake, wakipelekwa kuzikwa na Serikali katika Eneo la Kama lililotayarishwa makusudi kwa ajili hiyo.
----
[Picha na maelezo: Yussuf Simai - Maelezo via ZanziNews blog]



No comments:

Post a Comment