KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Thursday 22 December 2011

JAJI (MSTAAFU) DAMIAN LUBUVA ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI


I nytt fönster
Skriv ut alla










 




















 Jaji(Mtaafu) Damian Lubuva kushoto akiwa na Jaji Mkuu mstaafu Augustino Ramadhani


PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji (Mstaafu) Damian Lubuva kuwa
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Aidha, Rais Kikwete amemteua Mheshimiwa Jaji (Mstaafu) Hamid Mahmoud
Hamid kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Bwana
Julius Benedicto Mallaba kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi.

Taarifa iliyotolewa leo, Alhamisi, Desemba 22, 2011 na Katibu Mkuu
Kiongozi, Bwana Phillemon L Luhanjo mjini Dar es Salaam imesema kuwa
uteuzi huo umeanza tokea Jumatatu, Desemba 19, mwaka huu, 2011.

Kabla ya uteuzi wake, Mheshimiwa Lubuva alikuwa Jaji katika Mahakama
ya Rufani Tanzania na baada ya kustaafu aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa
Baraza la Maadili ya Viongozi.

Mheshimiwa Lubuva anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mheshimiwa Jaji
Lewis Makame ambaye mkataba wake wa utumishi wa umma ulifikia mwisho
Julai, mwaka huu, 2011.

Naye Mheshimiwa Hamid alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kabla
ya kustaafu kwake na anachukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Mhe
Jaji Omari O. Makungu. Mheshimiwa Jaji Makungu aliteuliwa na Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na baadaye
akateuliwa kuwa Jaji Mkuu.

Naye Bw. Mallaba, kabla ya uteuzi wake, alikuwa Mkurugenzi wa Sehemu
ya Mikataba (Contracts and Treaties) katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu
wa Serikali. **Bw. Mallaba anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bwana
Rajabu Kiravu ambaye amemaliza mkataba wake wa utumishi Septemba,
mwaka huu, 2011.

Imetolewa na:

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

22 Desemba, 2011

No comments:

Post a Comment