Katika salamu zake kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro kutokana na ajali iliyotokea katika Mlima Mbalizi, ambapo watu wapatao 11 wanasadikiwa kupoteza maisha na wengine ishirini na moja (21) kujeruhiwa, Rais alitoa pole kwa ajali hiyo ambayo imesababisha msiba mkubwa mkoani humo.
Pia alitoa rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ali Nassoro Rufunga kuhusu ajali iliyotokea Kahama, ambapo watu watatu walifariki na wengine 23 kujeruhiwa.
Rais Kikwete ametuma salamu hizo akiwa anatarajia kuanza ziara ya kiserikali nchini Canada kuanzia jana hadi mwishoni mwa wiki hii baada ya kualikwa na Gavana Jenerali wa Canada, David Johnston.
No comments:
Post a Comment