KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Monday 28 May 2012


Ziara Ya Waziri Kigoda Kiwanda Cha Urafiki

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mh, Abdala kigoda akiongea na wajumbe pamoja na Viongozi wa kiwanda cha Urafiki jijini Dar es Salaam alipotembelea kiwanda hicho leo jijini Dar es Salaam ambapo aliziona changamoto nyingi zinazozikabili kiwanda hicho ikiwemo mishahara miidogo ya wafanyakazi na akaahidi kuzifanyia kazi.
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Diwani wa kata ya Ubungo  jijini  Dr es Salaam Mh, Bonifas Jacob  akieleza changamoto zinazo wakabili wafanyakazi wa kiwanda hicho pamoja na usimamiaji mbovu wa Kiwanda hicho mbele ya Waziri.
Baadhi ya wafanyakazi, Viongozi pamoja na wajumbe mbalimbali waliohudhuria kwenye ziara hiyo wakimsikiliza Mh, Waziri kwa umakini.
Naibu Meneja uchapishaji na utiaji rangi kwenye kanga Bw, Solomon Laban(kulia) akimuelekeza waziri namana mtambo huo wa utiaji Rangi unavyofanya kazi  akikagua baadhi ya Mitambo ndani ya kiwanda hicho.
Waziri akikagua uzalishaji wa kanga kiwandani hapo.
Mh. Waziri wa viwanda na Biashara akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa kiwanda hicho baada ya kumaliza matembezi.

No comments:

Post a Comment