KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Monday 12 March 2012

CCM YAZINDUA KAMPENI ZAKE KWA KISHINDO ARUMERU MASHARIKI


. Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu wa CCM, Benjamin Mkapa akizindua kampeni za CCM za uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru Mashariki jana katika Uwanja wa Ngaresero. (Picha zote na Bashir Nkoromo)
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa akimnadi mgombea ubunge wa tiketi ya CCM jimbo la Arumeru Mashariki, Sioi Sumari kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM za uchaguzi huo kwenye Uwanja wa mpira wa Ngaresero jana.
Wananchi wa Arumeru Mashariki wakiwa wamefurika kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM.
Pamela Sioi Sumari akimnadi mumewe Sioi Sumari wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo za CCM. Pamela ni mtoto wa Waziri Mkuu wa Zamani Edward Lowassa.
Masanja wa Orijino Komedi akifanya manjonjo yake mbele ya umati, wakati wa uzinduzi wa kampeni za CCM
Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama akizungumza.
Mratibu wa kampeni za CCM, jimbo la Arumeru Mashariki Mwigulu Nchemba akiongoza msafara wa waendesha pikipiki kuingia uwanjani kwenye uzinduzi kampeni za CCM. Kulia ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM Martine Shigella.

No comments:

Post a Comment