KARIBUNI

Pata habari za kila siku, burudani,matangazo, na mengineyo mengi pia unaweza kuacha maoni yako kuhusu tovuti hii.

Sunday 9 December 2012


Kikundi Cha Akina Dada Wa Precious Group Chazinduliwa Rasmi

 

Mwenyekiti wa Kikundi cha akina dada cha Precious Group 2012 Agnes Shayo hiza akimkabidhi zawadi ya saa ya ukutani Magreth  Chacha ambaye ni Mkurugenzi wa benki ya wanawake (TWB)aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa kikundi hicho na chakula cha jioni iliyofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Isumba Lounge zamani Jolly Club jijini Dar es salaam, ambapo wageni mbalimbani na wanakikundi wa Precious walijumuika pamoja katika uzinduzi huo.
 
Mwenyekiti wa Kikundi cha akina dada cha Precious Group 2012 Agnes Shayo Hiza akimkabidhi tuzo maalum mgeni rasmi  Magreth  Chacha ambaye ni Mkurugenzi wa benki ya wanawake (TWB) katika hafla ya uzinduzi wa kikundi hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Isumba Lounge jijini Dar es salaam, kulia ni Jane Mchau mwanakikundi ambaye alikuwa ni MC katika hafla hiyo

   
Magreth  Chacha ambaye ni Mkurugenzi wa benki ya wanawake (TWB) akizindua rasmi kikundi cha Precious Groupkwenye ukumbi wa Isumba Lounge jijini Dar es salaam.
  
Magreth  Chacha ambaye ni Mkurugenzi wa benki ya wanawake (TWB) akifurahia jambo na  kikundi cha Precious Groupmara baada ya kukizindua rasmi usiku huu kwenye ukumbi wa Isumba Lounge.
  
Hapa ikabaki kuwa furaha kwa wote mara baada ya uzinduzi huo.
  
Magreth  Chacha ambaye ni Mkurugenzi wa benki ya wanawake (TWB) akiwapa nasaha wanakikundi wa Precious Group mara baada ya juzindua kikundi chao.
  
Mwenyekiti wa Kikundi cha akina dada cha Precious Group 2012 Agnes Shayo akizungumza na kukaribisha wageni katika hafla hiyo.
  
Christina Nyerere mshauri wa kikundi cha Precious Group akisoma risala mbele ya mgeni rasmi katika hafla hiyo.
  
Magreth  Chacha ambaye ni Mkurugenzi wa benki ya wanawake (TWB) akijadiliana jambo na Mweka hazina msaidizi wa kikundi hicho katika hafla hiyo, kulia ni Mwenyekiti wa Kikundi cha akina dada cha Precious Group 2012 Agnes Shayo

No comments:

Post a Comment